USIKATE TAMAA WEWE NI MSHINDI

Recent News

Friday, October 26, 2018

Kagere, Kichuya watapata tabu kwa Mbelgiji

Kiungo mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya na mshambuliaji Meddie Kageree wanatarajiwa kupata ugumu wa namba baada ya Kocha Mkuu, Patrick Aussemss kufanya mabadiliko ndani ya kikosi hicho kwa kuwahamisha Emanuel Okwi na Claytous Chama kucheza viungo wa pembeni.

Aussems amesema kuwa anataka washambuliaji wenye uwezo wa kufunga mabao na siyo kingine hivyo atatoa nafasi kwa wachezaji wenye uchu wa mabao wanapofika kwenye lango la wapinzani.

"Mimi hivi sasa nguvu na akili zangu ninazielekeza kwenye ufungaji pekee ambazo nimezianza kwenye mchezo na Alliance, nitahakikisha timu yangu inapata mabao mengi, kama mshambuliaji atakosa umakini nitamtoa.

"Ninafurahia kumuona Okwi na Chama wakifunga mabao kutoka pembeni hivyo ndivyo ninavyotaka, kama unakumbuka katika mchezo wangu na Stand United Kichuya na Kagere walishindwa kufunga, nataka wajifunze kupitia wenzao.

Kichuya hadi sasa amefunga bao moja pekee akiwa amecheza michezo  nane tangu ligi kuu imeanza amefanikiwa kuanza katika kikosi cha kwanza isipokuwa katika mchezo uliopita dhidi ya Alliance alikaa benchi, huku Kagere akiwa na mabao 4
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();

Author Details

Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.

Support

SUBSCRIBE OUR CHANEL