USIKATE TAMAA WEWE NI MSHINDI

Recent News

Friday, October 26, 2018

Mzee wa miaka 76 afariki baada ya kujinyonga

Mzee anayenufaika na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Tasaf, Anthony Mikami (76) amejinyonga kwa kamba ya chandarua katika kijiji cha Nyabihanga kata ya Bukiriro wilaya ya Ngara mkoani Kagera kwa kile kinachodaiwa kuwa na msongo wa mawazo

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyabihanga, Eradius Batakanwa amesema mzee huyo alijinyonga kwa kujitundika kamba kwenye mti mbali na makazi ya watu na aligundulika jana Jumatano Oktoba 24, 2018 saa 9:30 mchana kwa waliokwenda mabondeni kuvuna maharage.

Batakanwa amesema siku za hivi karibuni wakati wa uhai wake akiwa mnufaika wa Tasaf kijijini humo aliunguliwa na nyumba wakati akichoma viroboto na kuiteketeza nyumba hiyo.

"Baada ya kuunguliwa nyumba alichanganyikiwa maana alikuwa hana chakula cha usiku na mchana huku akiwa hana wasaidizi licha ya kujaliwa watoto watano wa ...kiume mmoja na wakike wanne," amesema Batakanwa na kuongeza kuwa hilo ni tukio la pili baada ya lile la kwanza lililotokea Februari.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();

Author Details

Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.

Support

SUBSCRIBE OUR CHANEL